BENKI YA DUNIA KUISAIDIA AFRIKA DOLA MILIONI 57

Benki ya dunia imetangaza msaada wenye thamani ya dola bilioni 57.wa miaka mitatu kwa mataifa yaliyoko kusini mwa jangwa la sahara huku sehemu kubwa ya msaada huo utatumiwa katika kutoa dhamana kwa mikopo isiyo na riba kwa baadhi ya mataifa maskini zaidi duniani .
Rais wa Benki ya dunia Jim Yong Kim anasema udhamini huo wa kifedha utayasaidia mataifa ya Afrika kuwa na ukuaji wa kiuchumi , kubuni nafasi za ukuaji huo pamoja na kuyalinda dhidi ya hasara na mizozo ya kiuchumi 
Kiwango cha pesa zenye thamani ya dola bilioni 45 kitatolewa kwa mataifa hayo kupitia Jumuiya ya kimataifa ya Maendeleo, ikiwa ni kitengo cha Benki ya dunia kinachohusika zaidi na mataifa maskini zaidi duniani .
Msaada huo wa fedha utasaidia kuboresha miradi 400 inayoendelea katika mataifa yaliyoko chini ya jangwa la sahara, kuanzia ile inayohusika na maendeleo ya miundo mbinu , elimu, utoaji wa huduma ya maji safi na huduma za afya za msingi.

Lengo ni kubuni hali itakayoweza kuinua uchumi na wachambuzi wanasema msaada huu kutoka benki ya dunia, unaweza kusaidia kwa kiwango kikubwa kuimarika kwa mchakato wa kufufua uchumi wa mataifa hayo
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment