SHULE KUMI BORA, NA ZILIZOSHIKA MKIA KITAIFA MATOKEO YA 'FORM SIX'

Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetaja shule kumi bora ambazo zimeongozwa na shule ya sekondari ya Feza Girls ya Dar es Salaam ambayo imeibuka kinara kwa watahiniwa wake 67 kufaulu kwa kupata daraja la kwanza na la pili, ikifuatiwa na Marian Boys (Pwani) iliyoshika nafasi ya pili, Kisimiri (Arusha) imeshika nafasi ya tatu na Ahmes (Pwani) imeshika nafasi ya nne. Marian Girls (Pwani) iliyoshika nafasi ya tano, Mzumbe (Morogoro) nafasi ya sita, St Marry Mazinde Juu (Tanga) nafasi ya saba, Tabora Boys (Tabora) nafasi ya nane, Feza Boys (Dar es Salaam) nafasi ya tisa na Kibaha ya Pwani iliyoshika namba kumi.

Orodha ya shule kumi bora kitaifa katika matokeo ya mtihani wa kidato cha sita
Shule zilizoshika mkia ni Kiembesamaki ya Unguja, Hagafilo (Njombe), Chasasa (Pemba), Mwenyeheri Anuarite (Dar es Salaam), Ben Bella (Unguja), Meta (Mbeya), Mlima Mbeya (Mbeya), Al-Ihsan Girls (Unguja) na St Vicent(Tabora).
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment