MAMBO 10 YA KUZINGATIA WAKATI WA KUFANYA MAOMBI YA KAZI UTUMISHI KUPITIA MTANDAONI


Serikali ya awamu ya tano sasa imeanza kutangaza nafasi za ajira kwenye vitengo mbalimbali baada ya kipindi kirefu cha mpito kilichosababishwa na uhakiki wa watumishi hewa na wenye vyeti vya kughushi.
Ongezeko kubwa la wahitumu kuanzia ngazi ya cheti, stashahada na shahada limesababisha soko la ajira kuwa gumu sana, lakini pamoja na ugumu huo bado kuna wahitimu wengi hawajui hatua zinazopaswa kufuata wakati wa kuomba ajira.
Ikumbukwe kuwa kwa sasa serikali inatumia mfumo wa kielektroniki (recruitment portal) kutangaza nafasi za ajira na kufanyia maombi. Na yapo baadhi ya mabadiliko na mambo ya msingi ya kuzingatia kabla ya kuomba nafasi zinazotangazwa na serikali kupitia utumishi.

Haya ni maelekezo juu ya hatua zinazopaswa kufuatwa wakati wa kuomba nafasi za ajira kupitia ‘recruitment portal’
1. Muombaji anapaswa kuwa na vyeti vinavyohitajika wakati wa kufanya maombi N.B. result slip, transcript na affidavit havihitajiki kwenye mfumo huu.
2. Kama muombaji hana baruapepe ‘email’ unapaswa kufungua baruapepe yake mwenyewe na uhifadhi namba/neno lake la siri (password)
3. Mwombaji atoa copy vyeti vyote anavyohitaji kuvitumia wakati wa kufanya maombi  Mfano: cheti cha shahada, academic certificate ya kidato cha nne na cha sita; na cheti cha kuzaliwa.
4. Muombaji apige picha (passport size) kisha achukua ‘soft copy’ yake na kuihifadhi kwenye vifaa maalum vya kutunza kumbukumbu Mfano: kwenye flash, simu, laptop nk
5. Muombaji atatakiwa kuchukua vyeti vyako pamoja na nakala zake (copy) kisha apeleka kwa wakili au mahakamani kwa ajili ya kuhakikiwa na kugongwa muhuri wa kuthibitisha uhalali wa vyeti vyake.
6. Mwombaji achukue nakala zake za vyeti zilizogongwa muhuri wa wakili au mahakama na aviscani ilia pate ‘PDF’. Pia ahakikishe kila cheti kinakaa kwenye kumbukumbu yaake na kukipa jina linalotofautisha cheti hiko na kingine. Mfano: cheti cha kidato cha nne utakipa jina ‘form four’, cheti cha kidato cha sita unakipa jina ‘form Six’ n.k
7. Muombaji achukue ‘soft copy’ ya vyeti alivyo’scan’ pamoja na ‘soft copy’ ya picha ndogo ‘passport size’ aliyopiga mwanzoni kisha ahifadhi kwenye faili moja ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa wakati wa ku’upload’.
8. Muombaji aingie kwenye tovuti ya utumishi www.ajira.go.tz kisha aenda sehemu ya ‘recruitment portal’ halafu aingie kwa kutumia baruapepe yake aaliyoifungua hapo awali na neno/namba ya siri. Hapo muombaji aanze kujisajili kama mwanachama mpya. Aingize email yake na ataweka ‘password’ kisha utaanza kuingiza taarifa zako kama zinavyojionesha kwenye website. Mfano: taarifa binafsi, taarifa za taaluma, taarifa za ajira n.k.
9. Muombaji afahamu kuwa kila sehemu inayohitaji cheti hususani sehemu ya taaluma ahakikishe ame’upload’ cheti chake husika, na akimaliza hatua hizo, ukurasa ‘profile’ yake itaonesha siyo chini ya 90% kama muombaji amejaza vizuri taarifa zako na kuweka vyeti vyake.
Baada ya kumaliza haua hizo muombaji anakuwa tayari kwa kuomba nafasi za ajira zilizotangazwa kwenye tovuti hiyo kulingana na taaluma yako.
10. Namna ya kuomba, muombaji aandike barua ya maombi ya ajira kisha a’upload’ kwenye tangazo husika.
Hapo muombaji atakuwa tayari amemaliza kufanya maombi yake ya ajira, tayari kwa kuhudhuria usaili endapo muombaji atakua ametimiza vigezo vya kuitwa.


Share on Google Plus

About Unknown

4 comments:

  1. a signed application letter, hapa sijaelewa, yaan una isaini kwenye hard copy halafu unahiscan na kuiupload au vip? msaada tafadhali

    ReplyDelete
  2. Website ya utumishi inasumbua. baadhi ya vipengele avifunguki asa kwenye kipengele cha elimu

    ReplyDelete
  3. Kwaiyo kama sijapata cheti siwezi kutumia transcript kuomba kazi?

    ReplyDelete
  4. Mi sijaelewa passport size unaiatach sehem gani

    ReplyDelete