MOTO WAUNGUZA MABWENI YA WANAFUNZI KENYA

Wanafunzi saba wamefariki na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya moto kuchoma bweni la shule ya Moi Girls mjini Nairobi nchini Kenya. Waziri wa elimu nchini Kenya Fred Matiang'i amesema kuwa wanafunzi kumi waliojeruhiwa wamelazwa hospitalini huku wawili kati yao wakiwa na hali mbaya.
Baadhi ya Majengo ya Shule ya Moi Girls yakiwa yanaungua kwa moto

Maafisa wa habari wa shirika la msalaba mwekundu katika shule ya Moi Girls wameeleza kuwa takriban wanafunzi kumi hawajulikani waliko kufuatia tukio hilo Naye waziri Matiang'i amesema kuwa shule hiyo imefungwa kwa muda wa wiki mbili kupisha uchunguzi kuhusiana na sababu ya moto huo.
Waziri huyo ameeleza kuwa wanafunzi wa kidato cha nne wataendelea na masomo yao ifikiapo siku ya Ijumaa na watasaidiwa kuendelea na masomo yao wakati ambapo wanajianda kufanya mtihani wa kidato cha nne wa KCSE. Mkuu wa shule hiyo amewataka wazazi kuwachukua wanawao.
Kulingana na gazeti la Daily Nation nchini humo mwanafunzi mmoja wa kidato cha kwanza ambaye alikuwa miongoni mwa wale waliotibiwa baada ya kisa hicho alisema kuwa moto huo ulianza mwendo wa saa saba usiku.
Alisema kuwa bweni lililochomeka lilikuwa na wanafunzi wa kidato cha kwanza na kwamba kulikuwa na makelele ya wanafunzi waliojaribu kujinusuru mbalii na mkanyagano huku wasichana wakijaribu kuAlisema kuwa bweni lililochomeka lilikuwa na wanafunzi wa kidato cha kwanza na kwamba kulikuwa na makelele ya wanafunzi waliojaribu kujinusuru mbalii na mkanyagano huku wasichana wakijaribu kutoka ndani ya bweni hilotoka ndani ya bweni hilo
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment