BODI YA MIKOPO IMETOA VIGEZO VYA KUPATA MIKOPO, WATOTO WA VIGOGO KUKOSA

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu nchini Tanzania (HESLB) imetoa vigezo na sifa kwa waombaji wa mikopo ya elimu ya juu na kuainisha ni wapi hasa wanastahili kupata mikopo hiyo kwa kuzingatia vipaumbele vilivyowekwa, ambapo watoto wa vigogo kutotarajiwa kuomba mikopo hiyo.

Bodi hiyo ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) leo Agosti 6 imeanza kupokea maombi ya mikopo ambapo mwisho wa uombaji wa mikopo hiyo unatarajiwa kuwa tarehe 4 Septemba, 2017.

Bodi hiyo imetoa vigezo kumi vya msingi kwa waombaji wa mikopo ya elimu ya juu, ambavyo ni;
  • Mwombaji awe Mtanzania
  • Mwombaji awe ameomba kudahiliwa na chuo kikuu au taasisi ya elimu ya juu inayotambuliwa na serikali
  • Asiwe mwanafunzi wa masomo ya jioni
  • Asiwe na udhamini/ufadhili/msaada wa kifedha kutoka katika vyanzo vingine
  • Awe ameomba mkopo kupitia mfumo wa mtandao (OLAMS)
  • Awe amefaulu mitihani ya mwisho wa mwaka (kwa wanaoendelea na masomo) na matokeo yake kuwasilishwa bodi ya mikopo na chuo chake
  • Awe amemaliza kidato cha sita au awe na sifa linganishi (kama Diploma n.k) ndani ya miaka (2015/12-2017/18)
  • Awe na umri usiozidi miaka 30 wakati wa kufanya maombi
  • Waombaji ambao wazazi wao ni wakurugenzi au mameneja waandamizi katika makampuni binafsi yanayotambuliwa na mamlaka za mapato na usajili hawatarajiwi kuomba
  • Waombaji ambao wazazi wao ni viongozi wa umma au kisiasa ambao wanatajwa na sharia ya maadili ya viongozi wa umma hawatarajiwi kuomba mikopo

Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment