RAIS WA AFRIKA KUSINI JACOB ZUMA APONEA CHUPUCHUPU

Rais wa Afrika kusini Jacob Zuma ameponea chupuchupu kung’olewa kwenye kiti cha urais kufuatia kura ya kutokuwa na imani naye zilizopigwa bungeni leo baada ya wabunge wengi wa chama tawala cha ANC kumuunga mkono.
Rais Jacob Zuma
Jumla ya kura zilizopigwa zilikuwa ni 384, wabunge 177 walipiga kura ya kumuondoa madarakani rais Zuma kwa kutokuwa na Imani naye, wabunge 198 walipiga kura ya kumuunga mkono huku jumla ya kura tisa zikiharibika.
Wafuasi wa rais Jacob Zuma walishangilia ushindi huo kupitia vigelegele na kucheza densi. Hata hivyo wabunge 40 wa chama tawala cha ANC walipiga kura ya kutaka kumng'atua mamlakani kulingana na mwandishi wa BBC Milton Nkosi kupitia ujumbe wake wa Twitter.
Chama cha upinzani nchini humo Democratic Alliance kinasema kuwa wabunge wengi wa chama tawala cha ANC walipiga kura hiyo wakizingatia maswala ya ufisadi.
Lakini ushindi wake ulikuwa mdogo , ikimaanisha kwamba idadi kubwa ya wabunge kutoka chama tawala cha ANC iliunga mkono muswada huo wa upinzani kumuondoa madarakani.

Kura hiyo ya kutokuwa na Imani na Rais Zuma inapigwa mara ya nane sasa tangu rais huyo aingie madarakani huku msukumo mkubwa ukitoka kwa waandamanaji na vyama vya upinzani vinavyotaka Rais huyo ang’atuke kwa kile kinachodaiwa kukithiri kwa vitendo vya kifisadi vinavyofanywa na Rais huyo na seikali yake. 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment