ZIMBABWE KUJENGA CHUO KIKUU CHA KUMBUKUMBU CHA ROBERT MUGABE

Serikali ya Zimbabwe imetenga jumla ya Dola za kimarekani Bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa chuo cha kumbukumbu cha Rais wa nchi hiyo Robert Mugabe  kwa ajili ya utafiti na uvumbuzi wa kisayansi na kiteknolojia ambacho kinatarajiwa kujengwa mjini Mazowe.
Rais Robert Mugabe
Akizungumza na waandishi wa habari leo Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Jonathan Moyo amesema Chuo Kikuu cha Robert Gabriel Mugabe kitakuwa chuo cha kwanza kwa kuwa na miundombinu kwa ajili ya masomo ya sayansi, uhandisi na teknolojia kwa asilimia mia moja.  
“Wizara imeridhika na maamuzi ya serikali kuanzisha Chuo kikuu cha Robert Mugabe, hautotambulika uwajibikaji wa Rais Mugabe kwenye elimu” amesema waziri Jonathan
“Tunapanga kufanya kazi pamoja na taasisi ya Mugabe Foundation na Chuo Kikuu cha Zimbabwe kuanzisha Chuo cha Robert Gabriel Mugabe, kitakuwa chuo kitakachowezesha uvumbuzi wa kisayansi, kiuhandisi na kiteknolojia ili kuboresha hali ya maisha” amesema Waziri Jonathan
Mamlaka yenye jukumu la kusimamia uanzishwaji wa Chuo kikuu cha Robert Gabriel Mugabe ni Taasisi ya Mugabe Foundation ambayo wadhamini wake wakuu ni Rais Mugabe na mke wake Dr. Grace Mugabe



Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment