Raia wa Kenya wameshiriki oezi
la Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2017 jana tarehe 8 Agosti, ambapo kwa mwaka huu yapo
matukio ambayo hayajawahi kutokea mara kadhaa katika chaguzi kuu nchini humo.
Matukio hayo yameibua hisia na maoni tofauti kwa watu nchini humo ambapo
wafungwa, na wagonjwa mahututi pia walishiriki zoezi hilo.
![]() |
Mwanaume aliyejulikana kwa
jina la Patrick Atindo mwenye umri wa miaka 64 alifariki dunia baada ya kupiga
kura katika kituo ch Sule ya msingi Lela kaunti ya Kisumu, ambapo kabla ya
mauti Patrick alikimbizwa hospitali siku moja kabla baada ya kulalamika maumivu
ya kifua.
Mtoto wake Silvanus Ouma
alisema baba yake aliamka saa 11 asubuhi tayari kushiriki zoezi la kupiga kura
na aliondoka nyumbani akiambatana na mkewe Mary Atinda.
Tukio lingine ni lile la
wagonjwa ambao walikuwa mahututi kutolewa mahospitalini na kupelekwa kwenye
vituo vya kupigia kura, ambapo mwanaume mmoja alifikishwa katika kituo cha
kupigia kura akiwa na mashine ya kupumulia kwa kutumia gesi.
Mwanaume aliyefahamika kwa
jina la John Nyakundi mwenye umri wa miaka 53 katika kituo cha kupigia kura ha
Shule ya Msingi ya Dandora alifikishwa kwenye kituo hiko cha kupigia kura akiwa
na mtungi wa gesi kwa lengo la kupiga kura
Wagonjwa wengine wengi wao
wakiwa waliolazwa katika jimbo la uchaguzi la Runyenjes, huku wengine
wakionekana na mabandeji makubwa na dripu, wagonjwa hao walipewa kipaumbele cha
kupiga kura.
Huko katika kituo cha kupigia
kura cha Shule ya Mseto ya Sekondari Konyau alijifungua baada ya kusimama
kwenye foleni kwa Zaidi ya masaa matatu. Imeelezwa na Diwani wa kata ya Kapchok
anayemaliza uda wake kuwa mwanamke huyo alihisi uchungu akiwa kweny foleni huku
akikataa kuwahishwa hospitali kabla ya kupiga kura.
Mwanamke mwingine mwenye umri
wa miaka 33 alijikuta mimba ikitoka akiwa kwenye foleni katika kituo cha
kupigia kura cha Kuwit baada ya kuhisi uchungu wa kuzaa huku akiwa na joto kali.
Katika tukio linguine mke wa
Uhuru Kenya alikaa kwenye foleni kwa saa nne ili kupiga kura.
Kwa mara ya kwanza nchini
Kenya wafungwa walipata nafasi ya kupiga kura katika uchaguzi mkuu mwaka huu
2017. Katika gereza lenye ulinzi mkali la Kamiti, mkuu wa timu ya usimamizi wa
Uchaguzi wa Umoja wa Africa Thabo Mbeki alieleza kuwa tukio hilo ni hatua
kubwa inayoleta matumaini kwa wafungwa kuwa nao wanaweza kuwa mchango kwa jamii
![]() |
Kijana aliyejitolea usafiri kwa wanawake
wajawazito, wazee na vipofu kuwafikisha
vituo vya kupiga kura
|
0 comments:
Post a Comment