DEREVA WA TUNDU LISSU ASAKW3A NA POLISI DODOMA

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto amemtaka dereva wa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Antiphas Lissu, ajitokeze ili  aweze kutoa maelezo yake kuhusiana na tukio la kupigwa risasikwa bosi wake.
Mbunge Tundu Lissu.
Kamanda huyo amesema kwamba sababu ya kumtafuta dereva huyo aliyemtaja kwa jina moja la Adam ni kwa sababu alikuwa pamoja na majeruhi wakati tukio hilo linatokea lakini tangu kutokwea kwa tukio hilo dereva huyo hajaonekana.
"Tangu kutokea kwa tukio dereva hakuonekana. Lakini kupitia gazeti tumeona ameanza kufanya mahojiano jana. Sasa amewezaje kufika Dar es salaam  na Dodoma asifike. Sababu za kutoonekana hazifahamiki. Dereva huyo ni mtu muhimu kwetu katika kutoa ushahidi. Natoa 'notice' afike ofisi ya Mkurugenzi wa makosa ya jinai Dar au ofisi ya Mkuu wa makosa ya jinai Dodoma atupe taarifa zinazohusiana na tukio hili. Tunaamini anazo siri za tukio hilo.
Kamanda Muroto ameongeza kuwa "Sheria yetu inasema mtu aliye na taarifa akashindwa kuzitoa kwa jeshi la polisi atakuwa amefanya mako. Na kwa nini asitoe.
Pia Kamanda huyo alimtaka Katibu Mkuu wa Chadema Dkt. Vicent Mashinji kufika kwa RCO mjini Dar es Salaam ama Dodoma kutokana kauli yake kuwa katika uchunguzi wao wamewabaini wahusika.
Amemtaka kutoa taarifa kwa jeshi la polisi kwa sababu kuonekana kwenye magazeti haitoshi bali kushirikiana kama mwananchi ndiyo njia sahihi ya kuwabaini wahalifu.
Pamoja na hayo Kamanda Muroto ameongeza kuwa "Tukio hili lisichukuliwe kama mtaji wa kisiasa. Nimesikia chama fulani kinahamasisha watu kutoa damu. Nawaomba watulie watuachie polisi nafasi ya kufanya kazi yetu. Matokeo mengi yameshatokea ikiwepo mauaji ya Kibiti, Mauaji ya Askari wetu lakini jeshi la polisi lilifanya uchunguzi na kubaini".

G
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment