RUGE AELEZA MAKONDA ALIVYOVAMIA CLOUDS




Mkurugenzi wa vipindi na vipindi na uzalishaji wa Clouds Media Group leo amethibitisha kwamba RC Makonda alivamia katika ofisi za Clouds Media Group. Alizungum. Alizungumza hay oleo asubuhi katika kipindi cha Clouds360 mbali na hayo mkurugenzi huyo ameonesha kusikitishwa na tukio hilo na kwamba hakutegemea kama RC Makonda angefanya hivyo .

“Mtangazaji mmoja alinifuata akaniambia wamefanya mahojiano na mwanamke anayedaiwa kuwa amezaa na Askofu Gwajima lakini Gwajima mwenyewe hawajampata. Niliwaambia watangazaji kama hawajampata Gwajima basi kipindi hicho kisirushwe kwa kuwa hakina ‘balance’ na wamwambie Makonda”
“Gwajima alinipigia simu akisema amesikia kuwa kuna kipindi chake, nikamwambia kuwa hakitarushwa kwa sababu hatujasikia pande zote. Na nikampigia simu mkuu wa vipindi kumwambia ahakikishe kuwa kipindi hicho hakirushwi kwa vile hakijabalance”
“Ijumaa saa 5 usiku nikapigiwa simu na Afisa Rasilimali watu wa Clouds kuwa Makonda amekuja ofisini akiwa na askari na wana bunduki, mlinzi hakusita kumruhusu aingie kwa vile amemzoea Makonda, ila alishtushwa na askari wale waliokuwa na bunduki”
“Nilimwambia  mlinzi aende kule juu studio aone kuna nini na alipokwenda alimkuta Makonda anachukua kipindi kwenye ‘flash’ kasha akaondoka nayo, hakuna kijana yeyote aliyepigwa usiku ule lakini tatizo kubwa ni namna tukio lilivyotokea”
Akizungumzia kuhusus CCTV kamera, alisema ni kweli wana CCTV ofisini kwao kwa sababu ni chombo cha habari, japo hajui ni nani aliyerusha na kusambaza video inayomuonesha Makonda akiingia Clouds akiwa na askari wenye bunduki.
“Ni kweli pale Clouds na sijui kaachia nani zile video, Ni kweli tuna Cctv kila sehemu maana hili ni jengo la habari“
Lakini pia aliongeza kwa kusema kuwa wamekuwa na uhusiano mzuri na Makonda na serikali na hawataki uhusiano huo ufe bali kuendelea kuzitangaza ajenda za kimaendeleo zitakazoletwa na seriali.
“Sijutii ukaribu wangu na Paul Makonda lakini nakwazika na kuvunjiana heshima. Kitu kibaya ambacho kinaumiza moyo Makonda ametumia vibaya madaraka yake pamoja na urafiki wake kwetu. Makonda ni mdogo wangu sana anaweza kuniomba msamaha, akumbuke mm nawakilisha kundi la watu waliokosewa kwenye hili”
“Hatua ya maamuzi yetu bado tupo kwenye mashauriano hatutaki kupingana na ajenda za serikali kwa sasa, tutaamua cha kufanya. Sisi sio viongoz ni Wananch tuna zaid ya miaka 19 kama chombo cha Habari tunakaribisha Agenda zenye ubunifu njooni tujadiliane pamoja”.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment