VIROBA, SILAHA NA DAWA ZA KULEVYA VYAKAMATWA MKOANI KILIMANJARO


Jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro linawashikilia watu watano akiwemo mfanyabiashara Gerald Kimario ambaye anashikiliwa kwa kosa la kufanya biashara ya pombe aina ya viroba na kukutwa na vifungashio vya pombe hiyo. Watuhumiwa wane wamekamtwa kwa kosa la usafirishaji wa dawa za kulevya na unang’anyi.

Jeshi hilo mbali na kuwakamata watuhumiwa hao, limekata silaha, dawa za kulevya, pombe aina ya viroba ambayo imepigwa marufuku kuuzwa pamoja na vifungashio vyake, na gari aina ya Scania ambayo ilikuwa ikisafirishia dawa za kulevya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi ,Wilbroad Mutfungwa akionyesha silaha zilizomakamatwa pamoja na Dawa za Kulevya aina ya Mirungi na Bhangi.

Mkaguzi wa Kanda ya Kaskazini wa Mamlaka ya Chakula na Dawa,William Mhifadhi akitizama Pombe iliyopigwa marufuku ikiwa katika vifungshio vya plastiki

Dawa za kulevya aina ya Mirungi iliyokamatwa.

Sehemu ya Vifungashio vya Plastiki vya Pombe viivyoppigwa marufuku hivi karibuni.
Silaha aina ya Bastola zilizokamatwa na jeshi hilo

Misokoto ya Bhangi iliyokamatwa.


Baadhi ya Waandishi wa habari wakifuatilia taarifa ya Kamanda wa Polisi,(hayupo pichani.)

Mfanyabiashara wa vinywaji kwa jumla ,Gerald Kimario akiwa amebeba boksi la Pombe iliyofungwa katika vifungashio vya Plastiki baada ya jeshi la Polisi kukuta bidhaa hizo katika ghala lake  la kuuzia bidhaa zake.

Watuhumiwa wa matukio ya usafirishaji wa Dawa za kulevya pamoja na Unyang'anyi wakiwa mikononi mwa jeshi la Polisi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutfungwa akionesha gari lililokamatwa likiwa na mizigo ya Dawa za kulevya aina ya Milungi ,wahusika wakijaribu kuisafirisha.


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment