KOREA KASKAZINI IMESEMA ITAJIBU MASHAMBULIZI YA MAREKANI KWA NYUKLIA

Naibu waziri wa mambo ya nje wa Korea Kaskazini Sin Hong Chol amesema wataendele kufanya majaribio ya kurusha makombora kila siku huku akiitishia Marekani kwa kusema kama wanapanga mashambulizi ya kijeshi wao watajibu kwa nyuklia katika mtindo wanaoujuwa wao.

Wazii huyo amezungumza hayo alipokuwa akihojiwa na mwanahabari wa BBC John Sudworth
“Tutaendelea kufanya majaribio ya makombora, kila siku, mwezi na kila mwaka” akaongeza kwa kusema “kama Marekani inapanga shambulizi la kijeshi dhidi yetu, sisi tutajibu kwa nyuklia katika mtindo tuujuao sisi wenyewe” Alisema Sin


Kumekuwa na majibizano kati ya Korea Kaskazini kwa siku kadha tangu Marekani ipeleke Meli za kijeshi katika rasi ya Korea, hali hii imepelekea hali ya wasi wasi kati ya nchi hizo mbili na hata ulimwengu juu ya uwezekano wa kutokea vita kubwa
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment