RIDHIWANI ALAZIMIKA KURUDI JIMBONI KUTOKANA NA MAAFA YA MAFURIKO

Mvua zinazoendelea kunyesha katika baadhi ya maeneo nchini zimesababisha maafa katika maeneo kadha ikiwemo katika wilaya ya Chalinze ambako makazi ya watu yameharibiwa kutokana na mvua hizo, eneo la Chalinze mzee, Bwawa la umwagiliaji la Msoga na Shule ya Sekondari ya Imperial yameathirika na mvua hizo.

Mbunge wa jimbo la Chalinze Mhe. Ridhiwani Kikwete amelazimika kwenda jimboni kwake kushuhudia maafa hayo, pia ametoa pole kwa wakazi hao na kuwataka wawe wavumilivu katika kipindi hiki kigumu.

Mbunge huyo ameeleza kwamba madhara makubwa yaliyosababishwa na mafuriko hayo ni kuharibika kwa mashamba, nyumba za wananchi na kusababisha wakazi wa maeneo hayo kwa takibani kaya kukosa mahala pa kulala. 

Mbunge wa Chalinze Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyevaa kanzu) akitazama athari za mvua ambazo zimesababisha bwawa la umwagiliaji la Msoga kuharibika

Baadhi ya nyumba ambazo zimeathirika na maafa ya mvua Chalinze Mzee

Sehemu ya bwawa la umwagiliaji la Msoga ambalo limeharibiwa kutokana na mvua zinazoendelea jimboni humo


Nyumba iliyopo Chalinze Mzee ambayo imeharibiwa na mvua

Nyumba iliyopo Chalinze Mzee ambayo imeharibiwa na mvua
Baadhi ya nyumba ambazo zimeathirika na maafa ya mvua Chalinze Mzee

Mbunge Ridhiwani Kikwete akijaza kitabu cha mahudhurio pindi alipofika katika kijiji cha CHalinze Mzee


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment