Msanii wa muziki wa hip hop
hapa Tanzania maarufu kwa jina la Roma Mkatotili leo ameeleza kwa kina jinsi
tukio la kutekwa kwake na wenzake lilivyotokea mpaka kufikia kupatikana katika
kituo cha polisi Ostabei. Msanii huyo alitekwa siku ya Jumatano majira ya saa
moja usiku yeye na wenzake katika studio ya Tongwe ambapo ndiko anakofanyia
kazi zake za muziki.
Msanii Roma alieleza tukio
hilo leo mbele ya waandishi wa habari katika ukumbi wa habari maelezo, Roma
ameeleza kwamba siku ya tukio waliwajia watu studio wakiwa na silaha za moto,
waliwafunga pingu, vitambaa vyeusi usoni na kuwaingiza kwenye gari na
kuwapekelekwa sehemu isiyofahamika ambapo walifanyiwa mahojiano, na baada ya
kumaliza mahojiano walifungwa midomo,
miguu na mikono na baadae kutupwa sehemu isiyojulikana.
Roma aliendelea kusimulia kwa kusema, kwa kuwa wailkuwa wamefungwa iliwachukua muda kujifungua, lakini walifanikiwa
kujifungua na kuanza kutembea bila ya kujua wapi walipo na hatimaye walifanikiwa
kukiona kibao kilichoandikwa ‘UNUNIO’ ndicho kilichowasaidia kutambua kwamba
wapo Dar, Roma na wenzake walichukua pikipiki na kuelekea nyumbani kwake (Roma), lakini
kwa sbabu za kiusalama waliamua kwenda kuripoti kituo cha polisi, Alisimulia
Roma Mkatoliki
Hata hivyo Waziri wa Habari,
Sanaa, Utamaduni na Michezo Dkt. Harryson Mwakyembe ameonesha kusikitishwa na
tukio hilo na kuahidi kulifuatilia suala hiyo kwa ukarib. Pia waziri huyo
amezungumza na waandishi wa habari kuhusu changamoto ambazo wasanii wanakutana
nazo na kusema kwamba yeye kama waziri anawathamini sana wasanii na anathamini
kazi wanayoifanya kuiwakilisha Tanzania.
“Mimi nawathamini sana hawa
wasanii, wanapeperusha bendera ya Tanzania” alisema waziri Mwakyembe
Pia aliongeza kwa kusema
kilichotokea hakivumiliki maana si kitendo cha kawaida huku akisisitiza
kulifuatilia jambo hilo kwa haraka.
"Hiki kilichotokea siyo
hali ya kawaida kwa watanzania, hatuwezi kukubali kitu kama hiki kiendelee
kutokea,nitalifuatilia kwa ukaribu sana, nitajitahidi nipate majibu kabla ya
bajeti yangu Bungeni". Alisema Dk. Mwakyembe
Pia waziri huyo amewaomba
wananchi kutoamini maneno ambayo yanazungumzwa na watu bila ya kuwa na uhakika
wa mambo hayo, na amewataka waandishi na vyombo vya habari kuwahoji wasanii
bila ya kuwa na taarifa kamili kutoka kwake.
Naye msanii Roma mbali na
kuelezea tukio hilo kwa ufupi amesema mambo mengine hatoweza kuyazungumza kwa
sasa kwa suala hilo lipo mikononi mwa polisi na linafanyiwa kazi ili kupata
taarifa kamili ya tukio hilo
"Kwa kuwa tumeshatoa
maelezo yote polisi, leo sitaongea sana maana nikisema mengine itakuwa ni
kuingilia upelelezi" Alisem Roma Mkatoliki
0 comments:
Post a Comment