Dar es Salaam April 20,
2017: kumekuwa na taarifa za upotoshaji, hasa katika mitandao ya kieletroniki
ya kijamii, kuhusu thamani halisi ya hisa za Kampuni ya Vodacom Tanzania Plc
(VTL) ambazo zinauzwa kwa umma hivi sasa.
Kumekuwa na ujumbe mfupi
uliozungushwa tarehe 19 Aprili, 2017
ukionyesha kuwa thamani halisi ya Kampuni hiyo ni pungufu sana ya ile
inayoashiriwa na bei ambayo hisa zake zinauzwa.
Umma unatakiwa kufahamu
kuwa ukokotoaji wa thamani ya hisa
zinazouzwa umezingatia viwango vya kitaalamu vya kimataifa.
Kama ilivyoainishwa kwenye
kipengele 2.1 cha Waraka wa Matarajio, bei ya TZS 850 kwa hisa umepitishwa na
Wakurugenzi wa VTL kwa kuzingatia ukokotoaji na mapendekezo ya Mshauri
Kiongozi, uliofanywa kwa kuzingatia mwenendo wa uchumi wa Nchi, historia na mwelekeo wa biashara na faida wa Kampuni,
na mwenendo wa bei za hisa za makanpuni yanayoshabihiana na VTL katika masoko
mengine ya Afrika hususani Kenya (Safaricom), Morocco (Marroctel) na Africa
Kusini (Vodacom Group Plc.).
Ukokotoaji wa thamani
ulizingatia nguvu ya kibiashara ya Vodacom katika upeo wa kati na mrefu ambapo
Wakurugenzi wanaamini Kampuni inaweza kujiimarisha zaidi kutokana na mwenendo
wake katika siku zilizopita, kuisha kwa changamoto ilizopitia katika miaka ya
karibuni, ongezeko la mapato linalotokana na kupanuka kwa biashara zake katika
nusu ya pili ya mwaka 2017 (ulioishia tarehe 31 Machi, 2017), pamoja na
uwekezaji uliofanyika na unaokusudiwa kufanywa. Matokeo ya ukokotoaji
yalilinganishwa na mwenendo wa bei za kampuni zinazofanya biashara kama ya
Vodacom katika masoko mengine kama ilivyotajwa hapo juu, baada ya kuzingatia
tofauti za ukubwa wa soko na hali ya uchumi jumla.
Kwa kuzingatia matokeo ya
uchambuzi huu, bei ya TZS 850 kwa hisa imefikiwa baada ya kugawanya thamani ya
mtaji wa VTL kwa kiasi cha hisa kilichokwisha kutolewa.
Haihitaji utaalamu mkubwa wa
masuala ya masoko ya mitaji kugundua upungufu ulio katika ujumbe mfupi uliosambazwa
tarehe 19 Aprili, 2017.
Ujumbe huo unadai kuwa njia
ya kufahamu thamani ya kampuni ni kukokotoa thamani ya rasilimali za kampuni
baada ya kutoa dhima (Net Asset Value – NAV). Njia hii si sahihi kutumika kwa
ajili ya kukokotoa thamani ya kampuni inayoendelea na biashara (yaani going
concern), bali hutumika kwa kampuni inayofungwa (kufilisiwa) kwa lengo la
kufahamu uwezo wa kulipa madeni yake.
Tofauti na kampuni
inayofungwa ambapo hakuna hitaji la kuzingatia uzalishaji wa mapato ya siku
zijazo, uthamani wa kampuni inayoendelea
na bishara unazingatia zaidi uwezo wa kuzalisha mapato katika muda ujao. Kwa
hiyo, ni kawaida thamani ya kampuni kuwa kubwa kuliko thamani ya vitabuni ya
rasilimali za kampuni husika baada ya kutoa dhima.
Kwa mfano, wakati ujumbe
mfupi uliosambazwa unadai kuwa bei ya hisa za VTL ambayo ni takribni mara 3.8
ya thamani ya rasilimali zake baada ya kutoa dhima ni ushahidi wa udanganyifu,
hisa za Safaricom nchini Kenya ziliuzwa kwa bei ambayo ni mara 5.8 zaidi ya
thamani ya vitabuni ya rasilimali za kampuni hiyo baada ya kutoa dhima kwa
mujibu wa taarifa ya soko la hisa la Nairobi ya tarehe 18 Aprili, 2017.
Hii inaonyesha siyo tu
makosa yaliyobebwa na ujumbe huo mfupi bali pia upungufu mkubwa wa ufahamu wa
masuala ya uthamanishaji wa biashara na hisa za makampuni alionao mwandishi
wake.
wawekezaji kuzingatia
ushauri wa nguli wa uwekezaji katika masoko ya hisa, Warren Buffet wa Marekani,
kuwa:'Ni bora kununua kampuni ya bora kwa bei ya haki kuliko kununua kampuni ya
wastani kwa bei ya chini.'
Wawekezaji tarajiwa mnaaswa
kupuuza ujumbe huo wa kupotosha na usio wa kitaalamu.
Pamoja na hayo tuongezee muda WS kununua hisa.Kama mwezi zaidi
ReplyDeletePamoja na hayo tuongezee muda WS kununua hisa.Kama mwezi zaidi
ReplyDelete