WATANZANIA WAADHIMISHA MIAKA 53 YA MUUNGANO MJINI DODOMA

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeadhimimisha miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanizibar ambao uliunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ukio hilo la mmuungano lilifanyika mnamo mwaka 1964 April 26 ambapo lilijumuisha uchanganyaji wa udongo kutoka Tanganyia na Zanzibar katika uwanja wa Uhuru Dar es salaam.
Kama ilivyo miaka yote sherehe za muungano hufanyika huku zikipambwa na burudani kutoka vikundi mbali mbali vya sanaa, maonesho ya halaiki pamoja na maonesho ya makomandoo ya kuonesha ukakamavu na namna ya kumkabili adui, ambapo sherehe hizo kwa mwaka huu zimefanyika makao makuu ya cnhi mjini Dodoma ambako serikali iko kwenye mchakato wa kuhamia huko.
Katika maadhimisho hayo ya miaka 53 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuru ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye alihutubia mamia ya wananchi wa mkoa wa Dodoma waliohudhuria katika maadhimisho hayo mjini Dodoma.
Katika hotuba yake Rais Magufuli amewaonya wale wanaojaribu kutaka kuvuja muungano ya kwamba watavunjika wao "Nataka niwahakikishie mimi na Dr. Shein tutaulinda Muungano kwa nguvu zote, atakayejaribu kutaka kuuvunja atavunjika yeye" alisema Rais Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais mstaafu wa awamu ya pili Mzee. Ally Hassan Mwinyi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, John Pombe Magufuli akisalimiana na mke wa muasisi wa Muungano Mwl. Julius Nyerere  
Kikosi cha Makomandoo wa JWTZ wakifanya maonesho ya ukakamavu mbele ya amiri jeshi mkuu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa amesimama kwa ukakamavu na heshima ya hali ya juu wimbo wa taifa ulipokuwa ukiimbwa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akikagua gwaride

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na mke wa muasisi wa Muungano Mwl. Julius Nyerere  

Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment