Baa la njaa mchini Sudan ya
Kusini huenda likazidi kutokana na kuongezeka kuwapo na mahitaji ya chakula
huku upatikanaji wa chakula ukiwa finyu. Watu laki moja nchini humo
wanakabiliwa na ukosefu wa chakula huku miongoni mwa sababu zinazotajwa ni
mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yanayoendelea.
![]() |
Mtoto anayekabiliwa na
utapia mlo kutokana na ukosefu wa chakula
|
Taarifa hizo zimetolewa na
Umoja wa Mataifa kupitia mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa
Sudan Kusini Bw. David Shearer, pia ameonya kuwa endapo jitihada za makusudi na
haraka hazitachukuliwa njaa inaweza kuenea zaidi katika maeneo mengi nchini
humo.
Mmoja wa wahanga wa baa hilo la njaa nchini humo, ambaye pia ni mama wa watoto watatu, Maria Nyamuoka amesema muda mwingine hulalamika kwamba wanahisi njaa lakini hukosa cha kuwapa watoto hao,
“watoto hulalamika kila mara
kamba wanahisi njaa, lakini sina cha kuwapa” alisema Maria
Taarifa kutoka Umoja wa Mataifa zinasema watu
Milioni moja wapo kwenye hatari ya kukumbwa na baa hilo la njaa mbali na watu
laki moja ambao tayari wamekumbwa ukosefu wa chakula, pia imeelezwa kwamba
watoto alio chini ya umwi wa miaka mitano wako kwenye hatari kubwa zaidi ya
kuathirika na ukosefu wa chakula kutokana na kuwa na kinga dhaifu. Pia zaidi ya
watu Milioni 5 wanategemea chakula cha msaada nchini humo.
0 comments:
Post a Comment