KICHUYA, BLAGNON WAIPA SIMBA UBINGWA WA AZAM FEDERATION SPORTS CUP KWA MARA YA KWANZA

Simba Sports Club imeibuka Bingwa wa kombe la Azam Sposts Federation Cup (ASFC) baada ya kuichapa timu ya Mbao FC bao 2 kwa bila katika mchezo wa fainali uliochezwa kati ya Simba SC na Mbao FC katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.


Mechi hiyo iliyoonekana ngumu kati ya mahasimu hao wawili katika dakika tisini za kisheria za mchezo huo, na kumlazimu refa aliyekuwa akichezesha mchezo huo kuongeza nusu saa ya ziada ndipo ambapo ilipelekea kuwepo kwa unafuu wa mchezo huo kati ya timu zote mbili ambapo timu ya Simba SC ilijipatia magoli yake katika dakika hizo za nyongeza huku Mbao FC ikijipatia goli la kufutia machozi katika dakika hizo za nyongeza.
Mnamo dakika ya 95 ya mchezo huo timu ya Simba ilijipatia goli lake la kwanza kupitia mchezaji wake machachari kabisa wa kimataifa Blagnon huku goli la pili likifungwa na  Shiza Ramadhani Kichuya kwa mkwaju wa penati mnamo dakika ya 120. Nao Mbao FC walipata goli lao la kufutia machozi ambalo lilitiwa wavuni na mchezaji Ndaki Robert.

Klabu ya Simba inakuwa timu ya pili kutwaa kombe la Azama Federation tangu kuanzishwa kwake dada ya Yanga FC kuchukua kombe hilo katika msimu wa kwanza. Kufuatia ushindi wa leo Club ya Simba wanapata na kitita cha Tsh. Mil. 50 na nafasi ya kuiwakilisha Tanzania katika Kombe la Shirikisho barani Afrika
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment