KILABU YA YANGA YADAIWA TSH. MILIONI 300 NA WIZARA YA ARDHI


Klabu ya soka ya Dar es salaam Young African (YANGA) imethibitisha deni ambalo inadaiwa na wizara ya ardhi Shilingi Milioni 300 ikiwa ni kodi ya jengo la ofisi za kilabu hiyo.
Katibu mkuu wa Kilabu hiyo Charles Boniface Mkwasa amethibitisha suala hilo kuwa tangu mwaka 1997 kilabu hiyo haikuwah kulipa kodi ya ardhi na kusema kwamba wanafanya kila jitihada kuhakikisha wanalipa deni hilo

“Ni muda mrefu kodi hii ilikuwa haijalipwa, kipindi hicho kodi ilikuwa ni rahisi ;lakini miaka ya karibuni imekuwa ikiongezeka na kama ninavyosema na tunatakiwa kulipa Milioni 56 na laki 6 kwa mwaka. Sisi kama uongozi tunafanya jitihada kubwa za kuweza kulinusuru jingo letu na Mungu akijalia itawezekana ” alisema Mkwasa
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment