MAREKANI YAFANYA MAJARIBIO YA NDEGE ZAKE ZA KIVITA KOREA

Korea Kusini imesema ndege mbili za kivita za Marekani zenye uwezo wa kutupa mabomu ardhini zimeruka katika anga la rasi ya Korea. Ndege hizo mbili aina ya B1-B zimeshiriki pamoja na ndege za kivita za Korea Kusini.

Rais wa Marekani Donald Trump alisema kuwa yuko tayari kufanya mazungumzo na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un iwa mazingira yataruhusu kufanya hivyo, naye msemaji wa Ikulu ya Marekani amesema kwamba Mazingira kama hayo unaweza kutowakutanisha Trump na Kim.
Rais Donald Trump amesema kuwa Korea Kaskazini inafanya vitendo vya kukera kutokana na mpango wake wa kutaka kuendelea kufanya majaribio ya makombora ya nyuklia.
Nayo Korea Kaskazini imeendelea kuongeza kasi yay a kufanya majaribio ya Makombora yake na silaha nyingine za nyuklia japo Umoja wa Mataifa tayari umepiga marufuku nchi hiyo kuendelea kufanya majaribio hayo.

Pia Korea Kaskazini inaamini kwamba silaha zake za nyuklia zinaweza kuilinda nchi hiyo dhidi ya shambulio la kijeshi kutoka kwa nchi ya Marekani na kile kinachoaminika kuwa Marekani na Korea Kusini zinaweza  kuunganisha na kumuondoa madarakani Rais wa nchi hiyo Kim Jong-Un
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment