RAIS MAGUFULI AONGOZA WAFANYAKAZI KWENYE SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI MJINI MOSHI


Rais Magufuli ameongoza sherehe za maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani Mei Mosi, maadhimisho hayo yamefanyika katika uwanja wa Chuo Cha Ushirika Moshi MoCU na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais Mama Samia Sluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angela Kairuki, Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Jenista Joakim Mhagama, Rais wa Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tumaini Nyamhokwa na shirika la kazi Duniani ILO.
Rais Dkt.John Magufuli akiwa uwanja wa Chuo cha Ushirika mjini Moshi katika sherehe za maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani,kutoka kushoto Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John William Kijazi,Spika wa Bunge Job Ndugai, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Jenista Joakim Mhagama  Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Rais wa Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tumaini Nyamhokwa,Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki, na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadik.
Maandamano ya wafanyakazi yamejumuisha wafanyakazi kutoka ofisi, mashirika na idara mbalimbali za serikali yakiongozwa na wafanyakazi kutoka ofisi ya Mkoa wa Kilimanjaro
Katika hotuba ya Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo Mhe. Rais Dkt John Pombe Magufuli imezungumzia mambo kadha ikiwemo kumalizika kwa zoezi la uhakiki wa vyeti kwa 98% ambako kutapelekea kuwepo kwa ajira za kutosha kufikia 52,000 na kuongezeka kwa mishahara ya watumishi wa umma.
Pia Rais Magufuli amesisitiza kuwa atatoa ushirikiano kwa vyama vya wafanyakazi na kusema kwamba wafanyakazi kujiunga na vyama hivyo ni hiari nan i jambo la kisheria. Pia amewataka waajiri wote kuhakikisha kuwa wanwaptia wafanyakazi mikataba kwani hilo I jambo la kisheria na mwajiri asipofanya hivyo anakwenda kinyume na sheria.
Mbali na hayo Rais Magufuli ametangaza kuanzishwa kwa bima ya ajira ambayo muswada wake utakapokamilika utawasilishwa bungeni kujadiliwa ili u[itishwe. Amegusia suala la malimbikizo ya michango ya michango ya mifuko ya hifadhi ya jamii ambayo waajiri wamekuwa wakilimbikiza bila kuwasilisha kwenye mifuko hiyo, kuwa ni jukumu la kila mwajiri kuwasilisha michango hiyo kwa wakati, amesema kabla ya kuwawajibisha waajiri wengine, ameanza na serikali na tayari kiasi kikubwa cha deni la michango ya mifuko ya jamii limepunguzwa kwa kiwango kikubwa na ameahidi kulimaliza. 

Maandamano ya wafanyakazi wakipita mbele ya Rais John Magufuli katika Viwanja vya ushirika mjini Moshi katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani.




Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment