RAIS WA SUDANI KUSINI AMFUKUZA KAZI MKUU WA MAJESHI YAA NCHI HIYO

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amemfuta kazi mkuu w a majeshi wa nchi hiyo Jenerali Paul Malong, mpaka sasa hakuna sababu yeyote iliyotajwa kuachishwa kwake japo katika siku za karibuni maafisa kadhaa wa juu katika jeshi na serikali ya Sudan Kusini wamekuwa wakijiuzulu.

Jeneali Malong amekuwa akishutumiwa kwa vita vya kikabila dhidi ya watu wa makabila ambayo hayana nguvu nchini humo.
Rais Kiir alitangaza kumfukuza kazi mkuu huyo wa majeshi katika Televisheni ya Taifa ambapo amemteua aliyekuwa msaidizi mkuu wa utawala na fedha katika jeshi la Sudani Kusini  kushika nafasi hiyo ya ukuu wa majeshi ya nchini humo
Wananchi wa Sudan wanaamini kuwa mkuu wa majeshi Jenerali Malong ana nguvu na uwezo wa kiushawishi hivyo wanasubiri kwa hamu ni kwa namna gani aataitikia kuondolewa kwake katika nafasi hiyo na Rais Kiir.

Kumekuwa na upendeleo na mapigano ya vita vya kikabila nchini Sudani Kusini, huku makabila yenye nguvu yakiwatenga na kuwanyima nafasi watu wanaotoka katika makabila yasiyo na nguvu kisiasa na kiuchumi 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment