SAIDI MECK SADICKI, JAJI MAHAKAMA KUU WAACHIA KAZI, RAIS MAGUFULI ARIDHIA.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameridhia maombi ya kuacha kazi kwa viongozi, Ndugu Saidi Meck Sadiki ambaye alikuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Ndugu Aloysius Kibuuka Mujulizi ambaye alikuwa jaji wa mahakama kuu ya Tanzania na Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania na Ndugu Upendo Hillary Msuya ambaye naye alikuwa jaji wa mahakama kuu Tanzania.
Taarifa hiyo ya Rais kukubali maombi hayo imetolewa leo Jumatano Mei 16 na Katibu mkuu kiongozi Balozi John Kijazi ambapo ridhaa hiyo ya rais kukubali maombi ya viongozi hao kuacha kazi kuanzia tarehe 15 Mei 2017. 
Ndugu Saidi Meck Sadiki ambaye alikuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro
Ndugu Aloysius Kibuuka Mujulizi ambaye alikuwa jaji wa mahakama kuu ya Tanzania na Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania 
Ndugu Upendo Hillary Msuya ambaye naye alikuwa jaji wa mahakama kuu Tanzania. 


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment