SERIKALI YATOA VIBALI VYA AJIRA 15,000 KUFUATIA ZOEZI LA VYETI FEKI

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa vibali vya kuajiri watumishi 15,000 katika kada mbalimbali mwezi huu kufuatia zoezi la uhakiki wa vyeti vya watumishi ambalo limeleta upungufu wa watumishi serikalini na kupelekea baadhi ya huduma kudhoofu katika upatikanaji wake.
Zoezi hilo lililofikia tamati yake April 28 kwa awamu ya kwanza lilibaini jumla ya watumishi 9,932 wenye vyeti vya kughushi, watumishi 1,538 wenye vyeti vyenye utata kwa kuwa na watumaji zaidi ya mmoja, huku watumishi 11,596 wakiwa na vyeti ambavyo havijakamilika.
Watumishi 11,596  wenye vyeti pungufu wametakiwa kukamilisha zoezi la kuwasilisha vyeti hivyo kabla ya Tar 15 Mei mwaka huu na watumishi 1,538  wenye vyeti vyenye utata nao wametakiwa kuwasilisha ushahidi wa umiliki halali wa vyeti hivyo Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kabla ya tarehe 15 Mei.
Nalo zoezi la uhakiki wa watumishi wa wizara ikiwa ni awamu ya pili ya uhakiki linatarajiwa kukamilika kabla ya Tarehe 10 Mei 2017 

Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment