WATANZANIA WAPEWA OFA YA KUTEMBELEA HIFADHI ZA WANYAMAPORI BURE

Serikali kupitia wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira imetoa ofa kwa watanzania wote kutembelea hifadhi za mbuga za wanyama bila kulipa kiingilio kuanzia tarehe 2 hadi 4 ya mwezi Juni kufuatia maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani inayoadhimishwa Tarehe 5 Mwezi June Duniani kote. Ambapo  kwa mwaka huu 2017 kauli mbiu ya siku ya Mazingira ni “Connecting people to nature”
Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) inawakaribisha wananchi wote kuitumia ofa hiyo ambayo itajumuisha msamaha wa kiingilio na ada ya magari, ambapo katika hifadhi ya Kilimanjaro ofa itakuwa ni ya siku moja huku gharama za malazi, usafiri na huduma nyingine zinazotolewa na sekta binafsi zikiwa hazipo kwenye ofa hiyo.

Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment