ACASIA WAKUBALI KULIPA FEDHA WANAZOADAIWA NA SERIKALI

Kampuni ya Barick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acasia Mining Limited imekubali kufanya mazungumzo na serikali ya Tanzania kwa ajili ya kufanya malipo ya fedha ambazo kampuni hiyo inadaiwa na serikali ya Tanzania baada ya kufanya kazi bila kulipa kodi tangu kampuni hiyo ya Acasia ilipoanza kazi zake.
Hatua hiyo imefikiwa baada ya mazungumzo kati ya Mwenyekiti wa kampuni ya Barick Gold Corporation Prof. John L. Thornton na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam. Mazungumzo hayo yameshuhudiwa na Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Ian Myles pamoja na waziri wa Katiba na Sheia Mhe. Palamagamba Kabudi.

Prof. John L. Thornton amesema kampuni yake iko tayari kufanya mazungumzo na Tanzania yatakayozingatia maslahi ya pande zote mbili na kulipa fedha ambazo Tanzania ilipaswa kulipwa tangu kampuni ya Acasia ilipoanza kufanya kazi Tanzania.
Rais Magufuli naye amekubali kufanya mazungumzo na kampuni hiyo na kusema kwamba ataunda jopo la waaalamu watakaojadiliana na kampuni hiyo kufikia makubaliano ya kulipwa kwa fedha hizo.
Pamoja na hayo Rais Magufuli amevionya vyombo vya habari vinavyowataja marais wastaafu juu ya kuhusika kwenye sakata la mchanga wa madini na kusema kuwa katika ripoti zote mbili hakuna mahala kaika ripoti hizo palipowataja marais wastaafu.
“Nimesoma ripoti zote mbili hakuna mahali ambapo Mze Mkapa na Mzee Kikwete wameajwa, vyombo vya habari waache kuwachafua hawa wazee, wamefanya kazi kubwa ya kulitumikia Taifa letu, tuwaache wapumzike” Alisema Rais Magufuli
Mazungumzo hayo ni matokeo ya kazi iliyofanywa na wataalamu wa Madini na Miamba ambao waliwasilisha ripoti ya kiasi na thamani ya mchanga wa madini unaosafirishwa kwenda nje kwa ajili ya uchenjuaji pamoja na ripoti ya pili ambayo ilifanywa na wataalamu wa sheria na uchumi ambao waligundua mambo kadhaa ikiwemo upotevu wa fedha nyingi na mapato ya serikali pamoja na kuwepo kwa mikataba mibovu na sharia dhaifu za madini na shughuli za uchimbaji madini Tanzania. 

Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment