REAL MADRID KUKIPIGA NA MANCHESTER UNITED KUFUATIA USHINDI WA GOLI 4-1 DHIDI YA JUVENTUS

Timu ya soka ya Real Madrid ya Hispania itacheza mchezo wa UEFA Super Cup na timu ya Soka ya Manchester United kutoka Uingereza baada ya kuunyakua kombe la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwa goli 4 kwa 1 katika mechi iliyochezwa katika uwanja wa Cardif kati yao dhidi ya Juventus jana.

Kufuatia ushindi huo kilabu ya Real Madrid ya Uhispania inaweka rekodi ya kuwa kilabu ya kwanza kuchukua ubingwa huo mara mbili mfululizo.
Mabao ya timu ya Real Madrid yaliwekwa wavuni na Christian Ronaldo ambaye alifunga mabao mawili bao la kwanza likiwa mnamo dakika ya 20 na bao lake la pili katika dakika ya 64, mabao mengine mawili yalifungwa na Casemiro mnamo dakika ya 61 huku bao la mwisho likifungwa mnamo dakika ya 90 na mchezaji Asensio.  

Goli la Juvenus lilifunga na Mandzukic  mnamo dakika ya 27.  Mechi hiyo iliyochezewa Cardiff ilikuwa ya 19 kwa klabu hizo mbili kukutana, mechi zote zikiwa katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya/Kombe la Ulaya.

Mchezaji Cristiano Ronaldo mpaka sasa amefunga jumla ya magoli 600 katika club alizowahi kucheza pamoja na timu ya taifa, ambapo katika kilabu ya RealMadrid amefunga magoli 406, Manchester United amefunga jumla ya magoli 118, huku katika timu yake ya taifa akifunga jumla ya magoli 71 na Sporting CP akifunga magoli 5.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment