PESA ZA ESCROW ZAMPONZA NGELEJA


Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) imezikana pesa ambazo zilirudishwa na aliyekuwa waziri wa Nishati na Madini Mhe. Wiliam Mganga Ngeleja ikiwa ni sehemu ya mgawo wa ESCROW alioingiziwa kwenye akaunti yake na mfanaybiashara James Rugemarira ambaye hivi sasa yupo rumande kwa mashtaka ya ubadhirifu.
Waziri wa Nishati na Madini wa zamani Ngeleja aliwasilisha TRA kiasi cha Shilingi za kitanzania Milioni 40.4 Jumatatu iliyopita ambazo aliingiziwa kwenye akaunti yake huku akionesha nakala pamoja na risiti za miamala hiyo ya fedha na visibitishi vingine kuwa amezirudisha fedha hizo na ziko mikononi mwa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA).
Ngeleja alieleza sababu ya kurudisha fedha hizo kuwa ni kujiondoa kwenye kashfa za ufisadi ambazo angeweza kushutumiwa kutokana na kiasi hicho cha edha alichogawiwa na James Rugemarira bila ya kujua kuwa ni mgawo wa ESCROW.
Ngeleja ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Sengerema (CCM) aligaiwa Sh. milioni 40.4 na mfanyabiashara maarufu James Rugemalira ambaye mwanzoni mwa mwezi alifikishwa mahakamani akikabiliwa na mashtaka 12, yakiwamo ya kughushi na utakatishaji fedha.
Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) imekana kuwa hazitambui fedha hizo na kuwa, mamalaka hiyo ina jukumu la kukusanya mapato pekee na si vinginevyo
Akizungumza na Nipashe mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma wa TRA, Richard Kayombo alisema mamlaka hiyo inahusika na kuhakikisha serikali inakusanya kodi stahiki na siyo urejeshaji wa fedha za kashfa kama Escrow.
Kayombo alitoa ufafanuzi huo wakati alipoulizwa na Nipashe juu ya utaratibu rasmi uliopo wa urejeshaji wa fedha hizo endapo wanufaika zaidi wa mgawo wa Rugemalira watataka kufuata nyayo za Ngeleja.
Akifafanua zaidi juu ya suala hilo, Kayombo alisema TRA haihusiki na fedha zilizochotwa kwenye akaunti ya Tegeta Escrow kwa kuwa hazikuwa mali yake.
Aidha, Kayombo alisema TRA haiwezi kuzizungumzia fedha hizo kwa kuwa hazijawahi kuwa mali yake na kuelekeza watafutwe wenye fedha hizo kwa ufafanuzi zaidi.
“Fedha za Escrow zinaihusu vipi TRA? Tunawezaje kukaa na kuzungumzia fedha ambazo si zetu?” Alisema Kayombo. “Mimi nashauri watafutwe wenyewe wazungumze kama wanataka kurejesha… siyo sisi.”




Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment