HOTUBA YA MWAKA YA RC MAKONDA JUU YA UTENDAJI KAZI, ISOME HAPA

Ndani ya mwaka wangu wa uongozi wangu Dar, nimekumbana na changamoto mbili. Kwanza muda umekuwa hautoshi kuwahudumia wananchi
Changamoto ya pili, ni namna ya mazoea ya watumishi wa serikali katika kuwahudumia wananchi. Tatizo la kwenye Kata linamfikisha mtu Mkoani.

Tulifanya uhakiki wa silaha, hili limesaidia kupunguza matukio ya kutumia silaha na kuwamaliza waliokuwa wanajiita Panya Road.

Acha wanaonichukia waendelee kunichukia, sina sababu ya kupendwa na mtu lakini niwe na uhakika na safari yangu ya mbinguni.

Nawataka wakazi wa Dar es Salaam wajue kuwa hatufanyi tunayofanya sababu ya chuki na mtu, lakini kwa vile tunawatakia yaliyo mema.

Makundi 2 yaliyokuwa yanasumbua, ni wapiga dili wa bandari na wauza dawa za kulevya. Wapigaji wa bandari walikuwa wanashrikiana na TRA.

Mzigo ukija haulipiwi kodi na sokoni wanajipangia bei. Kundi la pili ni wauzaji wa dawa za kulevya. Walikuwa huwezi kushindana nao kwenye kununua kitu, na sisi tusio na fedha wadada hawakututaka. Kundi jingine dogo ni wenye maduka ya kubadilishia fedha. Tumeongea na Waziri wa fedha, tunayahakiki, wiki ijayo mtasikia moto utawaka.

Dar es Salaam tunataka kuanzisha mfumo wa kulipia kwa njia ya kadi. Hii itasaidia kila mtu kula kwa jasho lake na tupate kodi

yumba 70% Dar es Salaam zimejengwa bila vibali na kuifanya serikali kukosa mapato halafu kuna mijitu inajizungusha kwenye kiti ofisini.

Mtu ukipewa kibali cha kujenga ukianza mara watu wa 'fire' wanakuja, kidogo OSHA wanakuja, sasa unajiuliza kibali ulichopewa ni cha nini?

Nataka watendaji mjipange, ukitoa kibali, toa kibali kimoja chenye kila kitu (Manispaa, Zimamoto, OSHA) tuache huu mlolongo mrefu.

Mimi sina tatizo na idadi ya watu wanaonichukia, ninachohitaji ni kutekeleza majukumu yangu niliyopewa na Rais Dkt Magufuli

Nafahamu kuna wamiliki wa nyumba wamelipwa fidia wabomoe nyumba zao lakini wao wakapangisha kwa watu wengi, tutawashughulikia wote.

Tumepata msaada wa ekari tatu ambazo tutajenga kituo kikubwa cha kuwasaidia waathirika wa dawa za kulevya ili waondoke mitaani walipo sasa.

Vyombo vya habari navishukuru sana, haijalishi mliandika vibaya au vizuri, lakini kwa vile mliandika kuhusu dawa za kulevya, basi tupo wote.

Kuna watu tuliwakamata wakasema hawatumii dawa za kulevya, tulipowaweka ndani siku mbili hadi sauti ikabadilika wanataka kwenda hospitali.

Tunajua baadhi yenu tukiwaita mnatumia Colgate na Chumvi ili tukikupima tusione dawa za kulevya, tuna mbinu mpya ya kuwakamata msijisumbue.

Wauzaji dawa za kulevya najua mmepungua, wengine mmekimbia mnapigiana simu kuulizana hali imepoa?, kuanzia kesho kasi inaongezeka mara mbili
Kuna Mtanzania amewekwa rehani Brazil, ndugu yake kaja kakopa benki ya Posta kafungua duka la nguo. Ila thamani ya duka na mkopo haviendani.

Rais Magufuli ni zawadi kutoka kwa Mungu, na mara nyingi zawadi kama hizi hatuzielewi hadi muda wake utakapokwishi ndio tutakuja kumuelewa.


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment