KIKOSI CHA TAIFA STARS KITAKACHOINGIA KAMBINI

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) limetoa majina ya wachezaji 26 ambao watakuwemo katika kikosi cha timu ya taifa ambacho kinatarajiwa kuingia kambini mnamo tarehe 9 mwezi Machi mwaka huu wa 2017.
Kikosi hiko chenye wachezaji ishirini na sita wakitokea timu za ndani na nje ya nchi ikiwemo KRC Genk ya Ubelgiji anayochezea ,mshambuliaji Mbwana Samtta, AFC Eskistuna ya nchini Sweden anayochezea mshambuliaji Thomas Ulimwengu na Teneriffe ya nchini Hispan anayochezea kiungo Farid Musa.

Kwa timu za hapa ndani, wachezaji ambao wanatoka timu ya Azam FC ni wachezaji saba ambao ni AIshi Manula (Kipa), Shomari Kapombe (Mlinzi), Gadiel Michael (Mlinzi), Erasto Nyoni (Mlinzi), Himid Mao (Kiungo), Salum Abubakar (Mlinzi), Frank Damoyo (Mlinzi), timu ya Simba imetoa jumla ya wachezaji ambao ni Mohamed Hussein (Mlinzi), Abdi Banda (Kiungo), Jonas Mkude (Kiungo), Said Ndemia (Kiungo), Muzamil Yasin (Kiungo), na Shiza Kichuya (Kiungo), wachezaji kutoka timu ya Yanga ni Deogratius Munishi (Goli Kipa), Hassan Kessy (Mlinzi), Vicent Andrew (Mlinzi), Simon Msuva (Kiungo), timu ya Mtibwa Sugar ametoka Said Mohamed (goli kipa), Salim Mbonde (Mlinzi), Kagera sugar ametoka Mbaraka Yusufu (mshambuliaji), Ruvu shooting ametoka Abdularahman Mussa (Mshambuliaji), pamoja na Mwadui FC ambako ametoka mchezaji Hassan Kabunda (kiungo).

Hii ndio orodha kamili ya kikosi hiko;
GOLI KIPA
AIshi Manula (Azam FC)
Deogratius Munishi (Yanga SC)
Said Mohamed (Mtibwa Sugar)
WALINZI
Shomari Kapombe (Azam FC)
Hassan Kessy (Yanga SC)
Mohamed Hussein (Simba SC)
Gadiel Michael (Azam FC)
Vicent Andrew (Yanga SC)
Salim Mbonde (Mtibwa Sugar)
Abdi Banda (Simba SC)
Erasto Nyoni (Azam FC)
VIUNGO WACHEZESHAJI
Himid Mao (Azam FC)
Jonas Mkude (Simba SC)
Salum Abubakar (Azam FC)
Said Ndemia (Simba SC)
Frank Damoyo (Azam FC)
Muzamil Yasin (Simba SC)
Simon Msuva (Yanga SC)
Shizza Kichuya (Simba)
Farid Musa (Teneriffe, Hispan)
Hassan Kabunda (Mwadui FC)
WASHAMBULIAJI
Mbwana Samtta (KRC Genk-Ubelgiji)
Thomas Ulimwengu (AFC Eskistuna-Sweden)
Ibrahim Ajib (Simba SC)
Mbaraka Yusufu (Kagera sugar)
Abdularahman Mussa (Ruvu Shooting)

Hapa ndani msimu huu timu za Simba SC na Azam FC zimeonekana zikitoa idadi sare za wachezaji ambapo zimetoa jumla ya wachezaji saba kila timu, ikifuatiwa na timu ya Yanga ambayo na yenyewe imetoa jumla ya wachezaji wanne, nayo timu ya Mtibwa Sugar ikitoa wachezaji wawili, huku timu za Madui FC, Kagera Sugar, Ruvu Shooting zikitoa mchezaji mmoja mmoja.







Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment