Vyombo vya habari nchini Korea
Kaskazini, vinasema kuwa taifa hilo limefanyia majaribio injini moja kubwa
maalum yenye uwezo wa kurusha angani mtambo wa Satellite. Majaribio hayo
yamefanya baada ya siku chache ambapo nchi ya China kuionya Marekani kuhusu
korea Kaskazini kuhusu uzalishaji wa silaha za nyuklia.
Kiongozi wa nchi hiyo, Kim Jong Un, amenukuliwa akisema kuwa,
injini hiyo mpya itaisaidia Korea Kaskazini, kufikia uwezo wa kimataifa wa
kufyatuaji Satellite angani.
Wachanganuzi wanasema majaribio ya mtambo huo wa kurusha angani
roket ambayo bado haijathibitishwa pia itakuwa jambo la kuangaliwa kwa undani
katika nia ya Pyongyang kuunda zana za kinuklia zenye masafa marefu.
Tangazo hilo linatokea wakati wa waziri wa maswala ya nchi za
kigeni wa Marekani, Rex Tillerson, anapofanya mazungumzo na viongozi wa China
huko, Beijing.
Awali, Bwana Tillerson, aliionya Marekani kuchukua hatua za
kijeshi dhidi ya Korea Kaskazini, kwamba inaweza kuharibu mambo hata zaidi.
0 comments:
Post a Comment