MADAKTARI KUTOKA TANZANIA KUZUILIWA AJIRA KENYA


Mahakama nchini Kenya imeizuia serikali ya Kenya kuajiri madaktari 500 kutoka nchini Tanzania kutokana na kile kilichodaiwa ni ushawishi kutoka kwa chama cha madaktari nchini humo.

Chama hiko kilikwenda mahakamani kudai ya kwamba wapo madaktari 1,400 nchini humo ambao mpaka sasa hawana ajira, lakini pia wamelalamikia ufujaji wa pesa kwa kile kinachodaiwa kwamba madaktari hao watakaoajiriwa kutoka Tanzania watalipwa Tshs.  360,000 kwa siku.

Agizo hilo limetolewa na mahakama  ya kazi siku ya Ijumaa terehe.31 Machi, na litadumu mpaka ombi hilo litakaposikilizwa na kuchambuliwa.
“The leave is hereby granted, to quash the decision of the government ..to hire foreign doctors to be  deployed to Kenya” zimeandika nyaraka za Mahakama (MachiMachi 31)


Ni wiki kadhaa tangu mgomo wa madaktari nchini Kenya kuanza, ambapo walikuwa wakidai kuongezewa mishahara na kuboreshewa mazingira ya kazi ikiwemo kuongezewa vifaa tiba. Siku za hivi karibu serikali ya Tanzania ilikubali ombi la serikali ya Kenya la kuomba madaktari ambapo serikali ya Tanzania imeahidi kupeleka madaktari 500.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment