MAREKANI YAPIGA MARUFUKU VIFAA VYA ELEKRONIKI KUTOKA NCHI NANE ZA KIISILAMU


Marekani imepiga marufuku kwa muda vifaa vikubwa vya kielektoniki kama kompyuta za kupakata, kamera, iPads visiingizwe katika mizigo inayobebwa na abiria ndani ya ndege kutoka mataifa kadhaa ya Mashariki ya Kati.

Marufuku hiyo vifaa vyote vya kielektroniki (isipokuwa simu) kwa abiria kutoka nchi nane za kiislamu kuingia navyo nchini humo huku mashirka yatakayoathirika Royal Jordanian EgyptAir Turkish Airlines Saudi Airlines Royal Air Maroc Qatar Emirates Etihad Kuwait AirwaysSababu ya marufuku hiyo ya muda  haikufahamika mara moja na maafisa wa Marekani hawakutaka kusema chochote.


Taarifa iliyotumwa katika mtandao wa Twitter na shirika la ndege la Saudi Airlines na taarifa iliyofutwa ya shirika la Royal Jordanian ziliwafahamisha wateja wao kuhusu marufuku hiyo ya vifaa vya kielektroniki vilivyo vikubwa kuliko simu ya mkononi. Shirika la Royal Jordanian lilisema vifaa kama kompyta aina ya laptop, kamera na vifaa vya kuchezea DVD na michezo ya kielektoniki vitahitaji kuchunguzwa chini ya sheria mpya za serikali ya Marekani zinazoanza kutekelezwa leo. Simu za mkono na vifaa vya utabibu vinavyohitajika ndani ya ndege vitaruhusiwa.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment