Meneja wa Manchester United amesema
anaamini wasimamizi wa Ligi Kuu ya Uingereza hawajali maslahi ya klabu za
Uingereza zinazocheza ligi kuu za klabu Ulaya. United watakutana na Middlesbrough Jumapili saa sita mchana saa
za Uingereza.
Wataingia uwanjani saa 62 pekee baada ya kucheza mechi ya ligi
ndogo ya klabu Ulaya, Europa League, Alhamisi ambayo walishinda FC Rostov hatua
ya 16 bora.
Mourinho amesema una uwezekano mkubwa kwamba United watashindwa
na kwamba inafaa kuwa jambo la msingi kwamba mechi hiyo ilifaa kuanza saa kumi
na moja jioni.
"Hawajali hata kidogo," aliongeza Mreno huyo kuhusu
wasimamizi wa Ligi ya Premia.
Huwa kuna makubaliano kwamba klabu ambazo zinacheza mechi Europa
League hazipangiwi kucheza Jumamosi japo kutakuwa na mapumziko ya kimataifa
baada ya mwisho wa wiki imeifanya mechi hiyo ya United na Middlesbrough
kutochezwa Jumatatu.
Mechi hiyo ya Middlesbrough itatangazwa na BT Sport, ambao huwa
wanaweza kuonesha mechi ya saa sita. Mourinho amesema wasimamizi wa soka
mataifa mengine huwa wanasaidia zaidi klabu zinazocheza Ulaya.
"Nchini Italia, klabu zinazofika hatua ya muondoano na
kucheza Jumanne au Jumanne, wiki ambayo imetanguliwa huwa wanacheza Ijumaa.
Ureno, inayofuata, huwa wanapangiwa mechi zao Jumatatu," alisema.
0 comments:
Post a Comment