NYUMBA 36 KUBOMOLEWA MTO MSIMBAZI

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ameagiza nyumba 36 zibomolewe katika bonde la mto Msimbazi na maeneo mengine hatarishi, ili kuondokana na janga la mafuriko.
Makonda amezitembelea nyumba hizo katika Kata ya Bugurni kwa Mnyamani na Tabata, akiwa na vikosi vya ulinzi na usalama ambapo ameshuhudia maafa makubwa yakiwemo ya baadhi ya watu kupoteza mali pamoja na nyumba zao kujaa maji na nyingine kubomoka kufuatia mvua zilizoanza kunyesha mwanzoni mwa mwezi huu jijini Dar es salaam.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akiavuka mto ambao umefurika maji alipokuwa katika ziara yake hiyo

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam akitizama sehemu ya nyumba ambayo imeboboka kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha

Mkuu wa mkoa akiwa na kikosi chake wakati wa ziara ya kutembelea wakazi wa bonde la mto msimbazi kushuhudia maafa yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha
Pamoa na watu wengi kupoteza makazi, mali na wenigne maisha, jambo ambalo limemgusa RC Makonda na kufikia uamuzi huo wa kuiomba Halmashauri ya Ilala kuanza zoezi hilo la ubomoaji mara moja.
RC Makonda amesema kuna watu ambao tayari wamelipwa pesa kuhama maeneo hayo lakini cha ajabu wengine hawajaondoka na wengine wamewapangisha watu wengine kwenye maeneo hayo hatarishi, jambo ambalo serikali yake haiwezi kulikalia macho na kuagiza kubomolewa kwa nyumba hizo.
Pia amewataka wale ambao hawajahakiki taarifa zao kuhusu kupewa hifadhi baada ya nyumba zao kubomolewa wafanye hivyo kwa kwenda ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala kwa uhakiki huo.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment