WFP LAANZA UTARATIBU WA KUGAWA FEDHA KWA WAKIMBIZI BADALA YA CHAKULA

Shirika la mpango wa chakula Duniani WFP limeanza kutoa kiasi cha shilingi elfu 20 pesa taslimu za Kitanzania, sawa na dola tisa, kwa wakimbizi wa kambi ya Nyarugusu iliyopo mkoani Kigoma Magharibi mwa Tanzania, ambapo zaidi ya wakimbizi laki moja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Burundi wamehifadhiwa katika kambi hiyo.
Hii ni mara ya kwanza kwa wakimbizi kupewa msaada wa chakula kwa mfumo wa kupokea fedha tangu kuwepo kwa kambi za wakimbizi nchini Tanzania.
Eneo la kambi hiyo ya Nyarugusu imeonekana ikichangamka baada ya wafanyabiashara hususani wa mazo ya chakula wakiwa wametia kambi katika kambi hiyo, huku wakimbizi wakiwa hawana namna nyingine ya kupata chakula cha kila siku zaidi ya kununua kutoka kwa wafanyabiashara hao.   
Hata hivyo wakimbizi wengi wameonekana wakifurahia utaratibu huo wa kugawiwa pesa badala ya chakula kwa kile walichokidai kwamba hawakuwa wakipata fursa ya kupata chakula tofauti na kile wanacholetewa na shirika hilo. “tulikuwa tunapokea unga tulikuwa na malalamiko mengi, hatubadilishi chakula tunaibiwa kwenye mizani lakini sasa hivi hakuna kuibiwa kwenye mizani ” alisema mmoja wa wakimbizi.

Kwa upande wa wafanyabiashara pia imekuwa neema kwao kwa kuwa mauzo yameongezeka      “zamani tulikuwa unauza tunapata laki tano lakini kwa sasa hivi mauzo yameongezeka kwa siku unaweza ukauza hata laki nane”   alisema Sostheness Raphael mfanyabiashara kutoka upande wa Tanzania 

Naye Said Johari mkuu wa shirika la umoja wa mataifa la mpango wa chakula WFP ofisi ya Kasulu anasema “pale tulipokuwa tunagawa chakula tulikuwa tunachukua siku tano mpaka saba kumaliza ugawaji lakini kwa mgoa wa fedha ugawaji unatuchukua maximum siku tatu, kazi imekuwa rahisi”

Brigedia jenerali Emmanuel Maganga mkuu wa mkoa wa Kigoma amezungumzia suala la usalama, anasema “ muingiliano ni mkubwa sana tunay matarajio ya kuanzisha vitambulisho vya wakimbizi”
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment