MAREKANI KUANDAA SHERIA YA KUPIGA MARUFUKU KUJICHUA

Nchini Marekani kumezuka muswada wa kutunga sharia ya kuzuia upigaji penyeto (kujichua sehemu za siri) lengo la sheria hiyo ambayo hoja yake imetolewa na,Jesica Farar ambaye ni mwanachama wa Democrat katika bunge la wawakilishi wa jimbo la Texas  anasema ni kuwalinda watoto ambao hawajazaliwa kila mahali, anataka mwanamume atakayemwaga mbegu zake za kiume nje ya uke wa mwanamke ama kutengemezwa nje ya kituo cha matibabu kutozwa faini ya dola 100.
Iwapo mwanamume atapatikana na hatia kwa kumwaga mbegu hizo nje itachukuliwa kama kitendo dhidi ya mtoto ambaye hajazaliwa. ''Iwapo inaonekana kama hatua isio ya kawaida basi hivyo ndivyo inavyopaswa kuwa''alisema Farrar.
Jessica Farrar aliuwasilisha muswada huo nambari 4260 wiki iliyopita japo anajua hautaidhinishwa kuwa sheria,  amesema kuwa sio rahisi zaidi ya kuwawekea wanawake sheria kali za utoaji mimba katika jimbo la Texas wakati mtu anapochagua kutaka kutoa mimba.
Sheria ya hivi karibuni ilikuwa ile inayowashinikiza wanawake kuchagua kuzika ama kuchoma mabaki ya viinitete kutokana na mimba iliotoka ama ile iliotolewa. Wakati wa kusikizwa kwa muswada huo mnamo mwezi Agosti, Seneta wa jimbo hilo Don Huffines alisema: kwa muda mrefu sasa Texas imeruhusu viumbe visivyo na hatia kutupwa na uchafu. Iwapo tunachukulia hatua hizi na umuhimu mkubwa kwa sababu ya maisha ,basi, hatuwezi kupoteza hata mbegu moja.

Hoja hii inapingwa wazi wazi na baadhi ya watu, mtu mmoja alituma ujumbe wake katika mtandao wa Twitter akisema kuwa ''ni yai lililorutubishwa pekee ambalo linahitaji kulindwa akiuliza iwapo angeweza kutumia sheria hiyo dhidi ya wanawake walio katika hedhi.
Jimbo la Texas lina sheria kali za utoaji mimba nchini Marekani japokuwa mahakama ya juu ilibatilisha marufuku juu ya utoaji mimba.
Sheria hiyo inamaanisha kwamba kliniki zinazotoa mimba ni chache mno.
Kulingana na gazeti la Tribune katika jimbo hilo kulikuwa na kiliniki 19 za utoaji mimba mnamo mwezi Juni 2016, nyingi zikifanya kazi katika maeneo ya mijini.



Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment