Wachezaji wa Mancheste United wakiwa wamemzunguka refa baada ya mchezaji mwenzao kupewa kadi nyekundu. |
Shirikisho la soka nchini Uingereza FA
limeishtaki klabu ya Manchester United kwa kushindwa kuwadhibiti wachezaji wake
wakati wa mechi ya robo fainali ya kombe la FA siku ya Jumamosi dhidi ya
Chelsea.
Refa Michael Oliver alizungukwa na wachezaji wa United baada ya
kumpa kadi nyekundu Ander Herrera dakika 10 kabla ya muda wa mapumziko, katika
mechi hiyo Manchester United ilipoteza mechi hiyo kwa 1-0.
Kiungo wa kati wa nchi ya Hispania Ander Herrera alitolewa nje
baada ya kumchezea visivyo mara mbili mshambuliaji Eden Hazard wa timu ya
Chelsea.
Taarifa ya FA ilisema kuwa Manchester United inatakiwa kujibu
mashtaka hayo hadi kufikia saa kumi na mbili jioni, kwa saa za nchini
Uingereza.
0 comments:
Post a Comment