URUGUAY YAWA NCHI YA KWANZA KUHALALISHA UUZAJI NA UNUNUZI WA BANGI


Huko nchini Uruguay kuanzia mwei Julai mwaka huu bangi itaanza kuuzwwa kwenye maduka ya dawa na kuwa nchi ya kwanza duniani kuuza bangi kihalali. Mchakato wa kuhalalisha matumizi ya bangi nchini humo ulianza mnamo mwaka 2013 baada ya kupitishwa kwa sharia ya uuzaji na ununuzi wa bangi.

“Bangi itauzwa kwenye maduka ya dawa kuanzia Julai” alisema Msaidizi wa Rais wa Uruguay, Juan Andrr Roballo alipokuwa katika mkutano na waandishi wa habari.

Bei ya bangi itakuwa $1.30 kwa gramu moja, na wauzaji wa bangi watatakiwa kujisajili nan i lazima wawe raia wa nchi hiyo au wakazi wa kudumu, haitaruhusiwa kwa muuzaji kununua gramu 40 kwa kipindi cha mwezi.

Mashamba ya bangi yatasimamiwa na serikali japo kwa watumiaji wa bangi wataruhusiwa kupanda majumbani mwao. Mpaka sasa tayari maduka 16 ya kuuza bangi yameshasajiliwa na maduka mengI zaidi yanatarajiwa kusajiliwa.


Hata hivyo wafanyabiashara wa bangi wameingia hofu juu ya kupata faida ya biashara hiyo kwa kuwa tayari serikali imepanga bei ya kuuza bidhaa hiyo, pia wameonesha kutokubaliana na serikali juu ya kupangiwa kiwango maalum cha kununua bangi kwa mwezi, wametaka wasipangiwe juu ya hilo.

Katika iku za karibunii nchi kadhaa ikiwemo Canada, zimeripotiwa zikijaribu kuhalalisha matumizi ya bangi kwa sababu kadha ikiwemo kile kinachosemekana kuwa ni tiba ya kansa
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment