Mbunge
wa Chalinze Mhe. Ridhiwani Kikwete ameandika katika ukurasa wa Instagram
kutokana na kutoweka kwa msanii Roma Mkatoliki na Moni ambao walitekwa siku ya
Alhamis majira ya saa moja jioni katika studio za Tongwe ambako amekuwa
akifanyia shughuli zake za muziki.
Mbunge
huto ameandika haya “Tabia hizi zinazoanza chipukia katika nchi vinapaswa
kukemewa kabla havijamea na kuzaa matunda. Mungu amsaidie kijana Roma na Moni
huko waliko” ameandika Ridhiwani
Ni
siku tatu sasa tangu tukio hilo ambalo limewashtua wengi kutokea, wasanii wa
muziki leo wamezungumza na waandishi wa habari pamoja na kujadili ni kwa namna
gani wanaweza kufanikisha kupatikana kwa Mwanahiphop huyo.
Nayo
serikali na vyombo vya usalama vimethibitisha kutoshikiliwa kwa msanii huyo na
wenzake na vyombo vya usalama. Kamanda Sirro kesho anatarajia kulitolea
ufafanuzi suala hili, ambapo awali ya yote jeshi la polisi limeomba kusaidiana
na wananchi kutoa taarifa ili kusaidia kupatikana kwa msanii huyo.
0 comments:
Post a Comment