BUNGE LATIKISWA NA UTEKAJI NA USALAMA WA WANANCHI

Baadhi ya wabunge katika bunge la Jmahuri ya Muungano wa Tanzania juu ya baadhi ya matukio ambayo yanatokea katika nchi ya Tanzanai ambayo yamepelekea kuwepo kwa hali ya sintofahamu kwa wananchi na wawakilishi wao juu ya mustakabali wa usalama wa maisha yao.

Jana April 11 katika bunge la Muungano wa Tanzania baadhi ya wabunge waliamua kutolifumbia macho na kuliongelea suala hilo, wapo waliotoa ushahidi wa chombo cha usalama wa taifa kuhusika moja kwa moja na baadhi ya matukio ya utekaji. Mbunge wa jimbo la Nzega Mjini, Mhe, Hussein Bashe kupitia Chama Cha Mapinduzi alitoa ushahidi kwamba yeye aliwahi kukamatwa na usala wa taifa na kuteswa,

“Mimi nimekamatwa na kuteswa na Usalama wa Taifa. Nimenyanyaswa sana nchi hii. Ikibidi mnifukuze” alisema Hussein Bashe

Hussein Bashe

Hata hivyo ni siku chache zimepita ambapo Bashe alisema kwamba wapo wabunge 11 ambao usalama wao upo hatarini kutokana na kupokea jumbe za vitisho, na kusema kwamba yeye ni mmoja kati ya wabunge hao ambao wamekuwa wakitumiwa jumbe za vitisho

Mbunge wa Sumbawanga mjnini Mhe Hillary Aeshi naye alitoa ushahidi juu ya viitisho ambavyo amewahi kutolewa na kupelekea kutoingia katika mkoa wa Dar es salaam,
“Mimi ni miongoni mwa wabunge niliotishwa na Mkuu wa mkoa wa Dar, na mpaka sasa mimi sikanyagi Dar licha ya kuimisi sana” alisema Hillary Aeshi

Aeshi

Lakini pia mbunge wa Jimbo la Chalinze alitoa ushauri kwa serikali kutokaa kimya juu ya mambo kama haya ya sintofahamu ambayo yanawatokea wananchi, na kwamba yapo baadhi ya mambo amabyo yakitolewa tamko huwatoa hofu wasiwasi na wananchi,  

“Hakuna sababu ya Mwigulu kuendelea kukaa kimya wakati wananchi wanaishi kwa wasiwasi juu ya usalama wao. Kutoa kauli  kunasaidia kutoa hofu” alisema Ridhiwani 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment