Katibu wa Halmashauri kuu ya
CCM (NEC), Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga
amewataka makada waliyumbuliwa na Rais Dkt. Magufuli kuacha kulalamika na
badala yake wakubali mabadiliko hayo na kuheshimu maamuzi ya yaliyochukuliwa na
Rais dhidi yao.
Kanali Lubinga aliyasema
hayo alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa vyuo vikuu ambao ni wanachama wa
Chama Cha Mapinduzi mkoani Iringa
“Rais anapoteua kiongozi na
kumpa dhamana ni kwamba anaona kuwa unahitajika, lakini inapofika mahali
amekuondoa ujue mazingira yale huwezi kuyamudu na anakuokoa ili usipate laana.
Baadhi ya viongozi wameondolewa madarakani, lakini wamebaki wakilalamika mitaani
ovyo” alisema Kanali Lubinga.
Mbali na kuyasema hayo
Kanali Lubinga hakutaja majina ya baadhi ya viongozi ambao wamekuwa wakifanya
vitendo hivyo pindi wanapotolewa kwenye nyadhifa zao.
Hivi karibuni kumekuwa na
kauli mbali mnali kutoka kwa viongozi kadha ambao wamtolewa kwenye nafasi zao
walizoteuliwa na Rais Magufuli, lakini pia wananchi wamekuwa wakitoa hisia zao
na maoni yao juu ya maamuzi hayo ya rais nay ale ambayo yamekuwa yakizungumzwa
na baadhi ya viongozi ambao wametumbuliwa.
Haya yanatokea siku kadhaa
baada ya aliyekuwa waziri wa Habari, sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Nape
Nnauye ambaye nafasi yake imechukuliwa na Dkt. Mwakyembe, Nape ameonekana
akiandika kwenye mitandao ya kijamii na hata kuitisha mikutano kuzungumza na
wananchi kuhusu maamuzi hayo ambayo Rais ameyachukua.
0 comments:
Post a Comment