MAREKANI YAKERWA NA JARIBIO LILILOFANYWA NA KOREA KASKAZINI

Makamu wa Rais wa Marekani Mike Pence amesema muda wa kuendelea kufanya subira na Korea Kaskazini umekwisha, hii inatokana na kitendo cha Korea Kaskazini kutaka kurusha kombora la majaribio ambalo hata hivyo lilishindwa kuruka. Makamu huyo wa Rais ameyazungumza hayo alipowasili katika mpaka wa Korea Kaskazini na Korea Kusini, Pence aliwasili mjini Seoul Jumapili muda mchache baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio hilo la kurusha kombora.

Makamu wa Rais wa Marekani Mike Pence (wa kati) 

Bw. Pence aliwaambia wanahabari alipokuwa katika kijiji cha Panmunjom siku ya Jumatatu huko Korea Kusini, alisema "Kumekuwepo na kipindi cha subira, lakini kipindi hicho cha subira kimemalizika."

Kumekuwa na majibizano makali kati ya Marekani na Korea Kaskazini Siku za karibuni ambapo, amjibizano hayo yameleta wasi wasi uimwenguni kwa kuhisi, pengine vita inaweza kutokea.  

Korea Kaskazini imeishutumu Marekani juu ya vitendo vyake ambavyo vinasemekana ni vya kiuchokozi na kuionya Marekani juu ya hilo na kusema kwamba Korea Kaskazini ipo tayari kwa vita, upande wa pili Bw. Pence amenukuliwa akisema kuwa jaribio la makombora la Korea Kaskazini ni uchokozi.


Marekani imeahidi kushirikiana na nchi ya Korea Kusini kuhakikisha panapatikana suluhu kwa njia ya amani ili kuhakikisha usalama katika eneo la rasi ya Korea. 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment