CHINA KUPIGA MARUFUKU UFUGAJI WA NDEVU HADI KUWA NDEFU


Huko nchini China utawala wa Beijing umeendelea na harakati zake zinazolenga kuzuia ueneaji wa itikadi kali nchini humo kwa kuzuia ufugaji ndevu hadi zikawa ndefu kwa wanaume ambapo utamaduni huu upo zaidi na unatekelezwa katika dini ya Kiisilamu ulimwenguni kote. Kufuatia suala hili sheria zimepangwa kuanza kutumika katika jimbo la Xinjiang magharibi mwa China.
Mbali na hilo, pia hatua nyingine ambayo imepangwa kuchukuliwa ni kuzuia mavazi ya wanawake ambayo yanaziba uso yanayojulikana kama niqab, haya yote yameelekezwa zaidi katika jimbo la Uighurs ambako kuna idadi kubwa ya waislamu, ni mara kadhaa watu wa jamii hiyo ya Uighurs wametaka kuwa na mamlaka huru na kusababisha kuwepo kwa mvutano mara kadha baina ya watu wa jamii hiyo na maafisa wa polisi.  

Wanaharakati ambao wanapinga sharia hizo wanasema zinalenga kuangusha utamaduni wa jamii ya waisilamu wanaoishi Uighurs
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment