WAANDAMANAJI WACHOMA MOTO MAJENGO YA BUNGE


Waandamanaji nchini Paraguay wamevamia majengo ya bunge la nchi hiyo na kuchoma moto kwa kile kinachodaiwa, bunge hilo kupiga kura za kurekebisha katiba na kuruhusu rais aliye madarakani Horacia Cartes kuendelea kugombea tena.

Katika tukio hilo wapo baadhi ya watu ambao walijeruhiwa baada ya polisi kujaribu kuwatawanya waandamanaji hao katika eneo la tukio kwa kurusha maji ya kasi na kufyatua risasi kwa lengo la kuimarisha usalama katika eneo hilo.

Waandamanaji hao wanadai ya kwamba mabadiliko hayo yanaweza kuharibu misingi ya demokrasia katika nchi hiyo, lakini yapo matumaini makubwa ya muswada huo kukubaliwa kutokana na Rais huyo kuwa na idadi kubwa ya wabunge wanaotoka katika chama chake lakini pia muswada huo uko mbioni kuelekea katika hatua ya pili ambapo utapelekwa katika bunge la darasa la pili.


Sheria ya kutoruhusu marais nchini Paraguay kutogombea mara mbili ilipitishwa mnamo mwaka 1992 ili kuondoa kile kilichokuwa kikidaiwa ni udikteta wa rais kung’ang’ania kuendelea kubaki madarakani. 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment