LIJUALIKALI ASIMULIA YALIYOMKUTA GEREZANI UKONGA


Peter Lijualikali ambaye ni mbunge wa Kilombero kupitia tiketi ya CHADEMA amesema amepata heshima kwa kifungo ambacho alikuwa nacho japokuwa alikuwa akipata mateso makali alipokuwa gerezani, amesema kifungo hiko kimempa furaha kana kwamba amepata shahada ya udaktari (PHD)

Alieleza chakula cha dagaa ambacho alichokuwa anakula ya kwamba kilikuwa na mchanga nusu kikombe mara baada ya kuoshwa “Tulikuwa tunakula ugali wa dona ambao kwa mtu wa kawaida hawezi kula kwa sababu umechanganywa na magunzi” alisema Lijualikali

Alisema kuna sehemu ndani ya gereza ambalo linaitwa siyaki shari, eneo hilo hutumika kuwaadhibu wafungwa ambapo alipata kushuhudia mfungwa mwenzake ambaye alipigwa hadi kufikia hatua ya kutambaa

Akiendelea kuzungumza alisema kwa hadhi yake kama mbunge alipaswa kulazwa daraja la tatu ingawa aliwekwa katika eneo tofauti na kuliacha daraja hilo walazwe watoto waa viongozi, watuhumiwa wa meno ya tembo na raia wa China ambao hakutaja kesi ambayo iliwapeleka gerezani.

“Magereza kuna madaraja matatu la kwanza, la pili, na la tatu ambalo nilitakiwa kulazwa hummo ili nipewe ulinzi kutokana na hadhi yangu” alisema Lijualikali


Lijualikali aliyasema hayo jana mara baada ya kutoka nje ya jingo la Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam alimokuwa akitumikia kifungo hicho na kuahidi kwamba vitendo vyote ambavyo  hakuvitaja atakwenda kuvisema Bungeni Dodoma. 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment