Mchezo uliochezwa leo kati
ya Chelsea na Manchester United katika uwanja wa Old Traford ambapo Manhester
United ililinda heshima yake kwa kutofungwa katika uwanja wa nyumbani, kwa
kupata ushindi wa Magoli mawili dhidi ya Mahasimu wao Chelsea.
Kocha wa Timu ya Manchester
United Josee Mourinho ameusifu mchezo waliouonesha wachezaji wake na kusema
kwamba walionesha mchezo mzuri.
Japo timu ya Chelsea imetoka
kappa katika mchezo wa leo, lakini bado inashikilia nafasi ya kwanza ikiwa na
jumla ya pointi 75, huku Manchester United ikishika nafasi ya tano ikiwa
imepanda kwa pointi 60, ambapo ni tofauti ya ponti 15 kati ya timu hizo mbili.
Pia katika msimamo huo timu
ya Liverpool imeonekana ikipanda huku Manhester City ikishuka daraja. Timu ya
Sunderland imeendelea kushika mkia ikiwa na jumla ya pointi 21.
0 comments:
Post a Comment