RAIS DKT. MAGUFULI AMEOMBA WAUMINI WAMUOMBEE

Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameomba waumini na wananchi wamuombee ili nchi iwe na umoja, amani, mshikamano na watu wenye kupenda kuchapa kazi, amezungumza hayo alipokuwa akishiriki ibada ya pasaka leo katika kanisa la Mtakatifu Petro akiwa pamoja na mkewe Mama Janeth Magufuli.

Ibada hiyo imeongozwa na Paroko wa Parokia ya Ostabei Padre Asis Mendokta na kuhudhuriwa pia na Askofu mkuu wa jimbo kuu Katoliki la Dar es salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo na waumini wengine.


Kardinali Pengo amemuombea Rais awe imara katika changamoto za kiuongozi anazokutana nazo, pia Kardinali Pengo amesema Baraka zilizoletwa na Yesu Kristo aliyefufuka ni kwa ajili ya watu wote na amemtakia Rais Magufuli heri ili matumaini ya Baraka hizo ziwafikie watanzania.   

Rais Dkt John Pombe Magufuli akisali ibada ya Pasaka katika Kanisa la Mtakatifu Petro jijini Dar es salaam leo Aprili 16, 2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea Mwili wa Bwana wakati wa ibada ya Pasaka katika Kanisa la Mtakatifu Petro jijini Dar es salaam.
Rais Dkt John Pombe Magufuli  akimuamkia Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo baada ya  ibada ya Pasaka katika Kanisa la Mtakatifu Petro jijini Dar es salaam leo Jumapili Aprili 16, 2017



Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment