Korea kaskazini imeshindwa
kufanya jaribio la kombora lake baada a kombora hilo kuripuka siku moja baada
ya maonesho ya silaha za kivita, kombora hilo lilijaribiwa kufyetuliwa lakini
lilishindwa kuruka angani.
Ni siku moja imepita tangu
nchi hiyo ya Korea Kaskazini kufanya maonesho ya silaha za kivita ambapo katika
shuhuli hiyo, Korea Kaskazini ilitoa onyo kwa Marekani juu ya vitendo vyake vya
uchokozi na kusema hawaogopi vitisho na ipo tayari kwa vita.
Matukio haya yanatokea ikiwa
ni siku kadhaa tu tangu Marekani ipeleke meli zake za kivita katika Rais ya
Korea.
Nalo jeshi la Marekani
limesema kuwa kombora hilo lililoripuka, lilitakiwa kurushwa sekunde chache
baada ya kufyetuliwa katika ufuo wa Mashariki mwa Korea Kaskazini.
Uhasama kati ya Marekani na
Korea Kaskazini umezidi kuongezeka kila uchao kwa siku za hivi karibu ambapo
kila mmoja kati yao amekuwa kionesha ubabe na jeuri ya kutaka kumuadabisha
mwenziwe.
0 comments:
Post a Comment