Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiaji
Prof. Kitila Mkumbo ametembelea Mtambo wa Ruvu Juu uliopo eneo la Mlandizi
Mkoani Pwani na kujionea kazi kubwa iliyofanywa na Serikali kupitia Wizara
anayoiongoza.
Akiwa
mtamboni hapo alipata fursa ya kushuhudia mtambo huo ukifanya kazi kama
ilivyotarajiwa baada ya upanuzi wake kukamilika, ambapo hivi sasa mtambo una
uwezo wa kuzalisha maji safi na salama kiasi cha lita milioni 196 kwa siku.
Akizungumza baada ya
kuhitimisha ziara yake Mkoani hapo, Prof. Kitila
amesema kwamba ziara hiyo ni muhimu kwake kwa kuwa amejifunza mambo mengi
kuhusu namna maji yanavyopatikana ambapo
ametoa pongezi kwa uwekezaji mkubwa uliofanyika katika eneo hilo.
“Uwekezaji huu ni mkubwa sana uliofanyika katika eneo hili, uwekezaji huu unahitaji kutunzawa ili kudhibti upotevu wa maji”, alisema Prof. Mkumbo.
“Uwekezaji huu ni mkubwa sana uliofanyika katika eneo hili, uwekezaji huu unahitaji kutunzawa ili kudhibti upotevu wa maji”, alisema Prof. Mkumbo.
Amewataka Mameneja wa Miradi ya Maji
kuhakikisha kuwa wanajiwekea malengo katika kuwahudumia wananchi na ametoa wito
kwa wananchi kuhakikisha kwamba wanayatunza maji wayapatayo kwakuwa upatikanaji
wake ni mrefu na Serikali imewekeza fedha nyingi katika kuyapata maji hayo.
\
0 comments:
Post a Comment